Waziri Mkuu Mstaafu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Fredrick Sumaye.
Sumaye ametoa kauli hiyo leo Novemba 26, 2019, wakati akizungumza na EATV na EA Radio Digital, iliyotaka kufahamu maoni yake juu ya orodha ya wagombea walioteuliwa na chama hicho hivi karibuni.
"Kwa sasa siwezi kuwaambia chochote nitaenda kuwaambia hukohuko ndani, ila nikishapita naombeni mnitafute ndiyo nije, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote kwa sababu nikifanya hivyo nitakuwa nimefanya tambo za kampeni ambazo mimi sitaki kufanya" amesema Sumaye.
Uchaguzi wa kanda kwa chama hicho unatarajiwa kufanyika Alhamis ya wiki hii ambapo wagombea mbalimbali majina yao yamepitishwa na Kamati Kuu ya CHADEMA ili kuwania nafasi hizo.