Mbunge wa Ubungo (CHADEMA), Saed Kubenea.
Akizungumza na www.eatv.tv akiwa njiani kuelekea kwenye ufungaji wa kampeni za ubunge wa Jimbo la Monduli Kubenea amesema hajaandika barua yeyote badala yake anaiona kupitia mitandao ya kijamii na kuongeza pia hajapokea barua yeyote kutoka kwa viongozi wa Chama chake ikimtaka kujieleza kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu
“Mimi sijui kuhusu hiyo barua na wala sijaiona .., kuhusu kuandikiwa barua na katibu mkuu mimi sijaiona na kama ipo haijanifikia", amesema Kubenea
Kupitia mkutano wa na waandishi wa habari Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Dk. Vincent Mashinji alikiri kuona barua ya mbunge huyo kupitia mitandao ya kijamii, huku akiweka wazi kwamba pindi itakapomfikia ataifanyia kazi.
Hivi karibuni Mgombea Jimbo la Ukonga Mwita Waitara alisema watarajie jambo lolote juu ya hatma ya Mbunge huyo wa Ubungo Saed Kubenea ndani ya CHADEMA.
Msikilize hapo chini Kubenea amefunguka zaidi.