Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif hamad, enzi za uhai wake
Dua maalum ya kumuombea Maalim Seif imeongozwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi, ambapo amesema kuwa msiba huu umeathiri watu wengi kwa sababu Maalim Seif alikuwepo kwa ajili ya Watanzania wote
Akizungumza wakati wa Dua hiyo Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum, amesema kuwa watu wanajua juhudi ambazo Maalim Seif, alizifanya na si kwa Wazanzibar pekee bali kwa Watanzania wote na kwamba ataendelea kukumbukwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.
Maalim Seif atazikwa leo Februari 18, 2021, huko Mtambwe, Pemba visiwani Zanzibar.