Mafuriko
Zaidi ya kaya 218 zenye wakazi zaidi ya 800 katika kijiji cha Isele hawana makazi baada ya kitongoji chao kufunikwa na maji huku nyumba zao zikisombwa na maji.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Isele, pamoja na Diwani wa kata ya Mlenge, Msafiri wameiomba serikali kuwanusuru wananchi na adha hiyo inayowakumba hivi sasa.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela amezungumzia juu ya madhara hayo na kuagiza Afisa Ardhi wa Wilaya kufika eneo hili kupima usawa wa ardhi pamoja na kugawanywa kwa maeneo ya ofisi za kijiji.
"Naagiza Afisa Ardhi kuja hapa kupima usawa kwa usawa wa kila kijiji, kugawanya eneo la ofisi za kijiji na ofisi za kujenga Kituo cha Afya na kuanzia leo ni marufuku mtu kujenga hovyuo hapa, pawe pakavu au pabichi", amesema Kasesela.
Kutokana na changamoto hiyo wito umetolewa kwa wasamalia kujitolea vifaa mbalimbali ili kuwasitili wananchi hao kutokana na changamoto inayowakabili.