Jumapili , 16th Feb , 2020

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema vijana wa Tanzania wapatao 497, wanaosoma katika vyuo mbalimbali vilivyoko kwenye mji wa Wuhan nchini China wote wapo salama.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

Kwa sasa Mji wa Wuhan umewekewa zuio hakuna mtu anayeruhusiwa kutoka wala kuingia, lengo likiwa ni kuzuia kuenea kwa maambukizi ya virusi vya corona.

Ametoa kauli hiyo leo Februari 16, 2020, kwenye Kumbukumbu ya Mazazi ya Mtume Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam iliyoandaliwa na Nida Textile Mills (T) ltd, na kufanyika katika Mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amesema kutokana na zuio hilo wakazi wote wa mji huo wakiwemo vijana wa Kitanzania, wanapata huduma mbalimbali kupitia njia ya mtandao. 

"Hakuna usafiri hata wa umma unaofanya shughuli za kusafirisha watu katika mji wa Wuhan kila mmoja anaetakiwa abakie katika makazi yake na kwamba Serikali ya China na uongozi wa vyuo unawatunza wanafunzi wote wakiwemo na Watanzania" amesema Waziri Mkuu.