Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
Akizungumza leo Januari 21, 2020, Makonda amekishukuru kiwanda hicho kwa kuamua kuunga mkono juhudi za Serikali, katika uboreshaji wa sekta ya elimu nchini.
"Mchango huu ni muhimu kwa sababu, Rais wetu anatoa elimu bure na kwenye Mkoa wetu takribani watoto 5,970 katika wilaya moja tu ya Temeke, walikosa madarasa na sasa tupo kwenye ujenzi wa madarasa 381, hivyo tuwashukuru wazawa kwa kuitikia mwito wa elimu, ndoo 500 zitakuwa ni mchango mkubwa sana ambao hauwezi kusahaulika" amesema Makonda.
Waziri wa TAMISEMI Seleman Jafo, aliwaagiza Wakuu wa Mikoa wote nchini kuhakikisha hadi kufikia Februari 28, 2020, wahakikishe wamekamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa ili ifikapo Machi 1, watoto waliokosa masomo kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa, waanze masomo yao.