Jumanne , 29th Mar , 2016

Sheria ya matumizi ya mitandao 'Cyber Crime Act ya mwaka 2015' pamoja na kurudiwa kwa uchaguzi wa Zanzibar kumefanya Marekani kupitia kwa shirika lake la ufadhili kutangaza kuzuia misaada yake ya kimaendeleo nchini yenye thamani ya dola 472.8 milioni

Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) imesema Tanzania haijatimiza viwango vinavyohitajika ili kunufaika na ufadhili kutoka kwa shirika hilo.

Mambo yanayolalamikiwa na shirika hilo ni pamoja na serikali kutochukua hatua za kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa na uguru wa kujieleza pamoja na utekelezwaji wa sheria ya uhalifu wa mitandao.

Aidha MCC imesema huwa inazingatia na kutilia mkazo demokrasia na kujitolea kwa nchi ili kufanikisha uchaguzi uwe huru na wa haki.

Fedha ambazo zimekuwa zikitolewa na MCC zimekuwa zikisaidia miradi mbalimbali ya kimaendeleo maji, umeme na barabara hasa maeneo ya vijijini ambapo kwa awamu ya kwanza serikali ilipokea Dola 698.

Chanzo BBC.