Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni.
Naibu waziri Masauni amezungumza hayo hii leo baada ya kuwatembelea majeruhi saba waliopo katika hospitali ya Micheweni, waliojeruhiwa baada ya kuzuka kwa vurugu katika eneo la Kwale, Wilaya ya Micheweni, Pemba, zilizohusishwa na itikadi za kisiasa ambapo amekemea vikali matukio hayo.
''Niwasihi sana wananchi kuepuka kuchochewa kuvunja sheria za nchi kuelekea katika uchaguzi mkuu sababu serikali imejipanga vizuri kuhakikisha kwamba atakayekiuka sheria za nchi basi sheria itafuata mkondo wake''amesema Masauni
Kwa upande wa Kamishna Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar, CP Mohammed Haji Hassan, amesema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ambapo watu 58 wanashikiliwa kutokana na tukio hilo.