Ijumaa , 24th Mei , 2019

Mkazi wa Kijiji cha Katoro na mfanyabiashara wa duka la nguo katika Kijiji jirani cha Nyarugusu mkoani Geita, Deus Mwenda(36) ameuawa kikatili kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali shingoni akiwa ndani ya duka lake.

Duka la nguo

Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku moja baada ya watuhumiwa 17 wa makosa mbalimbali waliokuwa wamehifadhiwa kwenye ukumbi wa jengo jipya la Mahakama ya Mkoa wa Geita wakisubili mashauri yao kutajwa, kudaiwa kutoroka.

Aidha tukio hilo limetokea majira ya mchana na kuacha maswali mengi kwa baadhi ya wafanyabiashara wenzake, kutokana na duka la mfanyabiashara huyo kuwa maeneo yenye msongamano wa watu na pembezoni mwa soko la kijiji hicho, ambapo wafanyabiashara hao sasa wameamua kufunga maduka kwa kuhofia usalama.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyarugusu, Amosi Yunge, mbali na kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo amesema tukio hilo limetokea saa chache baada ya mwanamke mwingine kubakwa na majambazi, huku mjane wa marehemu na ndugu wengine wakielezea jinsi walivyopokea taarifa za tukio hilo.