Jumamosi , 22nd Jun , 2019

Katika hali inayositaajabisha na kuacha maswali mengi, mwanamke mmoja mkazi wa Kitongoji cha CCM,Kijiji cha Buligi Kata ya Senga Wilayani Geita, Happnes Shadrack (36), anayedaiwa ni mgonjwa wa akili, amemuuwa mwanaye wa kumzaa, Martha Yakobo (1), kwa kumkatakata vipande vidogovidogo kisha

Picha haihusiani na tukio

 kumuweka ndani ya sufuria na baadaye kumpika kama kitoweo.

Tukio hilo limetokea majira ya saa saba za mchana,muda mfupi baada ya mtoto aliyeuawa kupelekwa kulazwa kwenye chumba cha bibi yake, kama dada wa marehemu anavyosimulia ambaye amedai kuwa alikwenda kumlaza ndani na yeye kwenda kucheza nje, baada ya muda mfupi alimuona mama yake akiwasha jiko na kudai kuwa alikuwa akichemsha maji.

Baadhi ya viongozi wa dini,akiwemo mchungaji Petro Mtani wa kanisa la Faith Mision akizungumzia unyama huo uliotendeka nyumbani kwa  Ruth Shadrack mama mzazi wa mtuhumiwa anasema.
 
Kaimu Kamanda wa polisi Mkoa wa Geita Kamishina msaidizi wa polisi Dismas Kisusi akithibitisha kwa njia ya simu kuwepo kwa tukio hilo amesema kuwa tayari mhusika amefikishwa kituo cha polisi na upelelezi unaendelea.