Kushoto ni picha za ajali na kulia ni Nape Nnauye
Nape amesema wananchi wa Kibutuka walifika eneo la ajali na kuwasaidia kuwatoa ndani ya gari pia wakawasaidia kulisukuma gari kwenda kulihifadhi katika kituo cha afya cha Kibutuka.
Ajali hiyo ilihuisha gari lake alilokuwa akilitumia aina ya Land Cruiser VX (nyeupe) lenye namba za usajili T349 DEL, ambalo liliacha barabara na kupinduka.
Mwenyezi Mungu kaniokoa na ajali mbaya leo asub, wakati natoka Mtama kuelekea kwenye kikao cha Chama Liwale. Namshukuru sana M/Mungu. Nawashukuru sana wananchi wa kijiji cha Kibutuka, wamenisaidia sana, Upendo wenu umenigusa sana! Familia,Viongozi na marafiki nawashukuru sana! pic.twitter.com/cldUXRqS9M
— Nape Moses Nnauye (@Nnauye_Nape) September 24, 2018
Nape alipata ajali hiyo akiwa anaelekea wilayani Liwale kuungana na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Taifa Dkt. Bashiru Ally anayezuru wilayani Liwale
Hata hivyo ajali hiyo haikuwa na madhara makubwa yaliyotokea kwa waliokuwa ndani ya gari. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi Renatha Mzinga alisema, eneo ilipotokea ajali hakukuwa na tatizo lolote hivyo uchunguzi zaidi unaendelea.