Ijumaa , 27th Mei , 2022

Rais Samia Suluhu Hassan, ametoa kibali cha kurekebishwa kwa posho ya kujikimu kwa safari za ndani ya nchi kwa watumishi wa umma kutoka Shilingi 120,000 hadi 250,000 kwa kiwango cha juu na shilingi 80,000 hadi 100,000 kwa kiwango cha chini.

Rais Samia Suluhu Hassan.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 27, 2022 na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishhi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro, na kwamba utekelezaji wake utaanza Julai 01, 2022.