Jumamosi , 17th Mar , 2018

Mkurugenzi wa mashtaka nchini Afrika Kusini amesema Rais Mstaafu wa nchi hiyo ambae alijiuzulu Jacob Zuma anatarajiwa kushtakiwa kwa makosa 18 ya rushwa dhidi yake.

Zuma mwenye umri wa miaka 75, alilazimishwa na chama chake cha African National Congress (ANC), kujiuzulu, amekana kufanya makosa hayo.

Mashtaka anayokabiliwa nayo Zuma yanahusu ununuzi wa silaha za serikali mwaka 1990 zilizokuwa na thamani ya dola za Kimarekani bilioni 2.5.

Zuma alikuwa anakabiliwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa mara ya 9 kabla ya kujiuzulu