Jumapili , 24th Jan , 2021

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa kesho Januari, 25 Tanzania inatarajia kupokea ugeni wa Rais wa Ethiopia Bi. Sahle-Work Zewde kwa ziara ya kikazi ya siku moja Wilayani Chato mkoani Geita.

Rais wa Ethiopia Bi. Sahle-Work Zewde.

Prof. Kabudi ameyasema hayo leo huko Chato wakati akizungumza na wanahabari kuhusu ujio huo wa rais wa Ethiopia ambapo amesema kuwa mahusiano ya Tanzania na Ethiopia yamekuwa ya shida na raha.

Uhusiano wetu na Ethiopia umekuwa katika hali zote na ni mahusiano ambayo yalitengenezwa na waasisi wa mataifa haya mawili ambayo yamekuwa na manufaa kibiashara,” amesema Prof. Kabudi.

Mhe. Sahle-Work Zewde ni rais wa kwanza mwanamke nchini Ethiopia.