Picha ikionesha jinsi Soko la Tegeta lilivyoteketea
Akizungumza na EATV &EA Radio Digital, Kamanda Kibona amesema kuwa tukio hilo la moto limetokea usiku wa kuamkia leo Februari 18, 2020.
"Moto usiku ulidhibitiwa lakini leo asubuhi tena ulishika kwenye vibanda Saba na sehemu ya mazao ya nafaka na wamefanikiwa kuuzima, tathmini ya kujua ni kibanda cha nani na ni hasara kiasi gani imetokea ndio inafanyika, na bado tunachunguza chanzo cha moto huo" amesema ACP Kibona.