Alhamisi , 21st Mar , 2019

Jiji la Mbeya limekumbwa na taharuki kufuatia kuzuka kwa tetemeko la ardhi lililodumu kwa zaidi ya sekunde 20 na kusababaisha sintofahamu kwa baadhi ya wakazi pamoja na viongozi wa mkoa huo.

Kwa mujibu wa mwandishi wa www.eatv.tv Grace Mwakalinga kutoka jijini Mbeya ameeleza tukio hilo lilitokea leo Machi 21, 2019 majira ya saa 5 asubuhi wakati viongozi wakuu wa mkoa wakiwa kwenye hafla ya siku ya elimu kwenye mkoa huo.

kwa taarifa za awali zinaeleza kuwa nyumba moja iliyopo mtaa wa Makunguru jijini humo imebomoka kufuatia tetemeko hilo.

Kwa taarifa kamili tazama video hapo hapo chini.