Mfano wa picha ya chemba inayotoa maji machafu
Wakizungumza na Kurasa hii leo wamesema eneo hilo limezungukwa na wafanyabiashara wa chakula hivyo uwepo ubovu wa chemba unapelekea ukosefu wa wateja kutokana na harufu mbaya inayotoka katika chemba na kuongeza kuwa washametoa taarifa kwa serikali ya Mtaa na DAWASCO lakini hadi sasa hakuna hatua zozote zilichokuliwa.
Aidha wameongeza kuwa chemba hiyo imebomoka kwa muda mrefu hali inayowatia hofu wakazi hao ambapo pia wamedai kuwa chemba imekua inaleta shida mara kwa mara japo viongozi wamekuwa hawalifuatilii kwa makini tatizo hilo.