Wanafunzi wa shule ya msingi Njinjo, wakiwa chini ya mti
Hayo wameyaeleza baada ya kusimamisha msafara wa Naibu Waziri wa TAMISEMI David Silinde, aliyekuwa anapita njia kutoka Kilwa Kivinje kukagua miradi mbalimbali ya serikali akielekea Liwale na kumuomba aone jinsi wanafunzi hao wanavyosoma chini ya miti.
Aidha wananchi hao wamesema kuwa mpaka sasa wamejitahidi kujenga madarasa matatu ambayo tayari wamekamilisha kuyajenga kwa nguvu zao pamoja na fedha milioni 30 kutoka halmashauri ya wilaya ya Kilwa na sasa wamepokea milioni 64 kutoka TAMISEMI ambayo wameambiwa wajenge madarasa matano na sasa wapo katika hatua ya uchimbaji wa msingi na kufyatua matofali.