Lengo la kurejea nchini mwao ni kusaidia mapambano dhidi ya vikosi vya Russia.
Mwezi March mwaka huu ilitanngzwa kwamba majeshi hayo yangerejea Ukraine huku onyo kutoka UN likisema kwamba ni hatari kwa usalama ikiwepo pia kuleta upungufu mkubwa wa rasilimali haswa helikopta.
Mapambano dhidi ya vikosi vya waasi wanaoipinga serikali ambao wapo kwenye misitu minene ya mashariki kwa Congo ni muhimu sana kwa sasa.
Helkopta 8 kutoka Ukraine huwa zinaunda sehemu kubwa ya majeshi ya kulinda amani ya umoja wa mataifa .
Tangu uvamizi wa majeshi ya Russia nchini Ukraine mwezi februari mwaka huu, nchi hiyo imekua kwenye mpango wa kuondoa majeshi yake kutoka kwenye vikosi vya umoja wa mataifa kwenye maeneo mbalimbali .

