Jumatano , 11th Jul , 2018

Utafiti umeonesha kuwa wanaume hasa vijana huwaza ngono muda mwingi kulinganiasha na wanawake au vijana wa kike kutokana na sababu za kisaikolojia.

Wanaume wa kiafrika

Akizungumza na www.eatv.tv mwanasaikolojia Dismas Lyaasa amesema kuwa wanaume kutokana na asili ya maumbile yao huwaza ngono kila baada ya sekunde tano mpaka saba.

"Kutokakana utafiti uliofanywa na taasisi ya uchunguzi wa masuala ya jinsia 'Kinsey Institute' kutoka Marekani chini ya daktari Alfred Charles Kinsey unaonesha kuwa mwanaume huwaza ngono mara mia tano kwa saa na mara elfu nane kwa siku sawa na saa kumi 16 ndani ya siku moja”, amesema Dismas

Aidha Dismas ameongeza kuwa jambo hili mara nyingi linawakumba wanaume ambao huelekeza mawazo yao kwa wanawake kila wanapokuwa karibu nao, na kwa ambao hawafanyi mazoezi ambapo miili ukaa kizembe na kusababisha ubongo kutopambanua mambo kwa wakati.

Hata hivyo Dismas amaeendelea kwa kusema matokeo ya jambo hili husababisha wengi kuanza kujihusisha na vitendo vya kujichua ‘masterbation’ na kupelekea wengine kuwabaka wapenzi wao au wasio wapenzi wao.