Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo.
Taarifa hiyo imetolewa leo Machi 20, 2020, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Mponjoli Mwabulambo, ambapo amesema kuwa mauaji hayo yametokea katika Wilaya mbili tofauti ikiwemo Masumbwe Wilaya ya Mbogwe, Mji mdogo wa Katoro na Mpomvu wilayani Geita.
Aidha Kamanda Mponjoli amesema kuwa hadi sasa Jeshi hilo linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kwa kuwa hakuna aliyekamatwa kutokana na matukio hayo.