Akitibitisha kutoka kwa tukio hilo, Mkuu wa wilaya ya Ubungo Bw. Kisare Makori amesema tatizo hilo limetokea baada ya kuwepo kwa hitilafu katika moja ya mtambo wa kuchuja tindikali lakini mpaka sasa, wamiliki wa kiwanda hicho wameshadhibiti na zoezi la uzalishaji linaendelea kama kawaida.
"Kuna watu watatu ambao walipata madhara zaidi yaani walikuwa wanatapika na kuumwa vichwa lakini wameshapatiwa matibabu na wengine 42 walienda katika kituo cha afya kupatiwa huduma kutokana na kuhisi kuathirika na hewa hiyo waliyoivuta wakati wakiwa kiwandani", amesema Makori.
Msikilize hapa chini Mkuu wa wilaya ya Ubungo Bw. Kisare Makori akisimulia zaidi..