Sehemu ya mitambo katika mgodi huo
Kufuatia ajali hiyo serikali imetangaza kuufunga mgodi huo kwa muda wa siku tatu, ili kupisha ukaguzi wa wataalamu wa madini katika mduara mgodini hapo.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, akiwa na Kaimu Afisa Madini Mkazi wa mkoa wa Simiyu, Mhandisi Amini Msuya na maafisa wengine wa serikali, wamefika katika mgodi huo na kutangaza zuio hilo.