Jumamosi , 9th Dec , 2017

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwene amemsimamisha kazi Mhandisi Goyagoya Mbena kwa tuhuma za kusaini barua ya kuruhusu ujenzi wa mradi wa Maji wilayani Nkasi mkoani Rukwa.

Taarifa iliyotolewa leo na Wizara hiyo, imeeleza kuwa Mhandisi Mbena amesaini barua kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo kinyume cha utaratibu hivyo Waziri Kamwene amemwagiza katibu kumsimamisha kazi mara moja ili kupisha uchunguzi.

Mradi huo wa Maji katika kijiji cha Kamwanda Halmashauri ya Nkasi mkoani Rukwa umeelezwa kuwa na thamani ya shilingi bilioni 7.4.

Chini ni taarifa ya wizara hiyo.