
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo
Amesema hayo leo Aprili 26, 2023 ambapo ametaja baadhi ya mafanikio hayo kuwa ni pamoja na kuimarika kwa uchumi, huduma za kijamii zikiwemo afya, elimu, maji na uanzishwaji wa Ofisi za Taasisi za Muungano Zanzibar.
Dkt. Jafo ametaja mafanikio mengine kuwa ni kuimarika kwa ulinzi na usalama, utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo kwa pande zote mbili za Muungano, utatuzi wa changamoto za Muungano, kuimarika kwa ushirikiano kwa masuala yasiyo ya Muungano na utoaji wa elimu ya Muungano kwa umma.
Amesema mafanikio hayo yameendelea kuwanufaisha wananchi wa pande mbili za Muungano na hivyo kuwezesha Muungano wetu kuendelea kudumu kwa zaidi ya nusu karne.
Ameongeza kuwa Muungano huu ni wa damu zaidi kwani wananchi wa pande zote mbili wanachanganyika na kufanya shughuli za kijamii pamoja bila kubaguana hivyo uemeendelea kudumu hadi leo.