Mwili wa aliyekuwa Mhashamu baba askofu wa Jimbo katoliki la Njombe Alfred Maluma ulipowasili uwanja wa ndege wa Njombe
Askofu Maluma alikutwa na umauti April 6 katika Hospitali ya taifa ya Mhimbili ambako alikuwa akipatiwa matibabu baada ya kupata ajali.
Mwili wake unatarajiwa kupumzishwa katika nyumba yake ya milele hapo kesho aprili 13 katika makaburi maalumu yaliyopo ndani ya kanisa kuu la mtakatifu Yosefu alipo kuwa akihudumu wakati wa uhai wake.