Bondia Mwakinyo akimchapa konde la uso mfilipino Arnel
Mwakinyo ametoa kauli hiyo, baada ya kuisha kwa pambano lake usiku wa kuamkia leo lililofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam, ambapo alimchapa Mfilipino, huyo kwa alama 97-93, 98-92 na 96-96.
Mwakinyo amesema kuwa"sipigi ngumi nyepesi napiga sana madude, kilichomsaidia Mfilipino alishasoma, alikuwa ananificha ukitaka kufanya finishing na yeye anapiga."
"Najua kitu kikubwa kilichokuwa kinambeba alikuwa mvumilivu sana, ila pia Mabondia wengi huwa tunapigwa nje ya nchi kwa namna ambavyo hata yeye mwenyewe amepigwa" ameongeza Mwakinyo