Jumamosi , 28th Mar , 2020

Kupitia show ya Friday Night Live ya East Africa TV inayoruka kila siku ya Ijumaa kuanzia 3:00 usiku hadi 5:00 usiku, MwanaHipHop maarufu hapa nchini Chidi Benz, ameomba msamaha kwa wananchi juu ya kuleta utani kwenye janga la ugonjwa wa virusi vya Corona.

Msanii wa HipHop Chidi Benz

Chidi Benz ameomba msamaha huo baada ya kusambaa kwa video mitandaoni ikimuonyesha anazungumzia ugojwa huo kwa njia ya utani kupitia chombo kimoja cha habari kwa kusema 

"Corona ni mafua ambayo yamekuwa ni mara mbili yake, watakaoathirika ni wale ambao mfumo wao wa pua utakua unashika vumbi kwa haraka ila kwa sisi Waafrika ukikamua mafua yanatoka kama keki Corona haipiti kokote

Aidha akiomba msamaha huo Chidi Benz ameeleza kuwa  "Kuhusiana na Corona ni ugonjwa ulio serious mtu yoyote asiuletee utani, mimi naomba msamaha kwa kile nilichokifanya kuhusu Ugonjwa wa Corona, ile niliongea kama utani tu ili nisichanganye watu".