Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Enock Bella
Enock Bella amebainisha hayo alipokuwa anapiga stori na www.eatv.tv na kusema kuwa sababu kubwa ya yeye kutokuwa na wivu na wakina Aslay, Beka Flavour pamoja na Maromboso ni kutokana hawapambani wao kama wao.
"Siwezi kujisikia wivu kutokana na mafanikio ya wenzangu waliyo kuwa nayo hadi hii leo, kwasababu wao wanafanya muziki kwa kusukumwa na mtu nyuma yao, bibi sina hao watu na badala yake ninatumia nguvu ya umma katika kukamilisha mambo yangu", amesema Enock Bella.
Pamoja na hayo, Enock Bella ameendelea kwa kusema kuwa "laiti ningekuwa na watu nyuma yangu wanahakikisha muziki wangu unaenda, siwafichi mimi ningekuwa mtu ambaye sifanani na yoyote kwa wasanii tuliotoka Yamoto Band, maana nina hazina kubwa ya kazi zangu".
Enock Bella ni miongoni mwa wasanii waliokuwa wanavutiwa na wengi wakati walipokuwa katika kundi la Yamoto Band kutokana na uzuri wa sauti yake ya 'base' lakini lilipokuja kuvunjika kundi hilo, ili mchukua muda mrefu hadi alipokuja kutoa kazi yake ya awali lakini hakuweza kupata mapokezi mazuri.