Khadija Kopa amesema anaamini CHADEMA haiwezi kumpa yeye nafasi ya uongozi kwa kuwa wanamjua vilivyoj jinsi alivyo CCM kindaki ndaki.
Aidha ameongeza kwamba "Kwani hawana demokrasia mpaka wanipe mimi? Kwani wanapeana peana tu. Akhaa najua hawawezi kunipa eti".
Mbali na hilo mkongwe huyo amedai hajawahi kufikiria kwenda chama cha upinzani kwani hajaona pa kwenda.
Akiizungumzia CHADEMA, Bi. Khadija amesema hakifahamu chama hicho zaidi ya kulisikia jina na bendera.