Juma Sharobaro
Juma Sharobaro ameileza EATV & EA Radio Digital kuwa anatumiwa message nyingi za kinadada hasa katika mtandao wa kijamii wa Instagram lakini kutokana na utamaduni wa Kichina, anatakiwa awe na mwanamke mmoja tu ambaye tayari anaye.
"Watu wengi wananitumia message, nafikiri kufuatana na utamaduni wa China inabidi nishikilie mtu mmoja tu kwa hiyo siwezi kuwa na moyo wa kutafuta mchepuko. Huwa wananitafuta ila siwajibu za Instagram ndiyo nyingi zaidi na kuhusu mastaa hiyo ni siri kidogo", ameeleza Juma Sharobaro.
Pia ameendelea kusema bado hajafikiria kuwa na mpenzi Tanzania kwa sababu ana mchumba wake ambaye ni raia wa China na anamtembelea mara kwa mara, japokuwa anaishi kwao China.