Msanii wa HipHop Bongo Mr Blue
Mr Blue amesema sasa hivi anajiona kama nyani mzee kwa sababu mama yake na ndugu wengi wa mama yake mzazi wametangulia mbele yaki na hata baba yake pia ametangulia kipindi yeye ana umri mdogo sana.
Aidha ameongeza kusema alivyokutana na hali hiyo alitaka kuchanganyikiwa na ilifika hatua alifikiria kuacha muziki, ila anamshukuru mkewe na mama watoto wake Wahda ambaye amemfanya kusahau hayo yote.
Ikumbukwe Mr Blue amewahi kusema mkewe Wahda anampenda sana kwa sababu amemvumilia wakati msanii huyo alipokuwa na wanawake wengine watatu ndipo alipoamua kumchagua yeye