Muimbaji wa Injili Joel Lwaga na mpenzi wake
Tukio hilo limefanyika Julai 26, limehudhuriwa na watu maarufu kama MC Pilipili ambaye alipost picha na video ya tukio hilo kwenye ukurasa wake wa Instagram pamoja na MC Luvanda.
Akizungumza na EATV & EA Radio mara baada ya kumchumbia mpenzi wake huyo Joel Lwaga amesema kuwa "Kuhusu ndoa watu wasubiri tamko langu, hayo ni mambo binafsi na nyeti kwa sababu yanahusiana na familia, kwa misingi yetu ya imani kuvisha pete ni hatua ya mapema ambayo haihitaji presha wajumbe watulie kidogo"
Zaidi tazama tukio lenyewe hapa chini.