muigizaji wa filamu nchini, Wema Sepetu
Hayo yameelezwa mbele ya Mahakama hiyo na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na kusema sababu kubwa ya kesi hiyo kuhairishwa ni kutaka kupata muda wa kupitia baadhi ya vitu vinavyohusiana na kesi ya msanii huyo.
Baada ya maamuzi hayo kutolewa Mahakamani leo Julai 16, 2018 www.eatv.tv ilifanya jitihada za kumtafuta Wakili wa Wema Sepetu, Alberto Msando na kusema kwamba kwa sasa hawezi kuzungumza jambo lolote dhidi ya kesi hiyo.
Wema Sepetu anakabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya bhangi, na kesi hiyo imehairishwa Julai 20, 2018.