Msanii wa BongoFleva Tunda Man akiwa na mkewe Sabra
Akizungumzia hilo Tunda Man ameeleza kuwa mkewe hajapokonywa gari ila kilichotokea ni kumuuzia gari Chief Kiumbe baada ya mke wake kudai gari hilo linamzidi kimo na linampa shida.
"Gari nilimuuzia Chief ninao hadi mkataba wa kumuuzia hadi pesa sijamaliziwa kama milioni 7 au 8 hivi, gari alitembea nalo mke wangu ila aliligonga na lilimzidi kimo tukalipeleka kwa fundi kisha Chief akalipia kulinunua,sasa hivi nimemnunulia gari nyingine yenye thamani ya Milioni 22, kwa sasa hivi Chief amekwama Afrika Kusini kwa sababu ya Corona ila alipanga akirudi aje kunimalizia" ameeleza Tunda Man