Wasanii wa BongoFleva Billnass na Nandy
Nandy ameeleza hilo kwenye show ya Dadaz ya East Africa TV, ambapo amefunguka mengi ikiwemo suala la mahusiano, kazi, bifu na wasanii wa kike, pamoja na historia yake ya muziki.
"Alivyonivalisha pete wiki nzima ilikuwa ni furaha na kupewa hongera tu, huku marafiki zangu na wake walikuwa wapo tayari kutoa michango ya harusi, kipindi tumeachana Billnass aliniambia ikitokea tunarudiana tutafunga ndoa moja kwa moja, hata ile kunivisha pete nilikuwa sijatemegea kama ingetokea mwaka huu, nataka harusi yangu iwe na watu 300 au 400 sio ya watu wachache kisa kuogopa Corona" ameeleza Nandy.
Zaidi tazama kwenye video hapa chini.