Msanii Baba Levo upande wa kushoto na Abdul Nondo upande wa kulia
Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, Baba Levo amesema hataki virusi katika jimbo lao na atapambana naye kuhakikisha analichukua jimbo hilo na ikishindikana bora aje alichukue mwenye jimbo lake Zitto Kabwe.
"Nilisema kama Zitto Kabwe hatagombea mimi nitagombea, nitapambana na mtu yeyote atakayekuja Kigoma Mjini, lengo ni kuzuia virusi na watu ambao hawana sifa za kuongoza, Abdul Nondo kutangaza nia ya kugombea ni Demokrasia lakini amenichukiza sana bora Zitto arudi kuchukua Jimbo lake wote tukose" amesema Baba Levo
Zaidi tazama kwenye Video hapa chini.