Shamsa Ford akiwa na Nay wa Mitego.
Video hiyo aliiweka Shamsa Ford, kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram, ambapo aliandika.
"Kuachana si bifu jamani mnaachana kwa amani na upendo na kila mmoja amuombee kheri mwenzie, sisi vijana na tunategemeana kwenye kazi nyingi za kujenga Taifa letu, ahsante kwa kuja binamu yangu" ameandika Shamsa Ford.
Kupitia EATV & EA Radio Digital, Shamsa Ford alipoulizwa kuhusu kama alikuwa anawasiliana na Nay wa Mitego, kipindi wameachana na hili ndilo jibu lake.
"Ndiyo, alinitania tu siku alivyosikia Ndoa yangu imeachika, akanipigia simu akaniambia 'Cousin' nasikia vitu vimeharibika huko" alijibu Shamsa Ford.