Jumatano , 20th Feb , 2019

Muigizaji wa filamu asiyeishiwa matukio mjini, Steve Nyerere amemvaa Irene Uwoya baada ya ku'post' picha ya mwanadada huyo iliyoonesha utofauti na kuandika ujumbe ulioacha maswali kwa watu wengi mtandaoni.

Kushoto ni Steve Nyerere pamoja na picha alizoziunganisha za Irene Uwoya.

Steve Nyerere ame'post' picha ya Irene Uwoya akiwa amefanya make up na nyingine akiwa hana make up na kusema kuwa ameingalia picha hiyo zaidi ya mara kadhaa na amekosa jibu.

Steve Nyerere ameandika “DAAAAAAAAAA Hiiiiiiiii LAST MINUTE. Walahi nimekuangalia mara 30000000000000000 nimejikuta nasema NO LONG PATISPET″.

Steve Nyerere amekuwa akitumia lugha ya Kingereza kwenye maongezi yake mengi, ambayo imekuwa ikichanganya wengi kutokana na kutumia misamiati ambayo huwa haieleweki kwa wengi kwa namna anavyoitamka na kuzua maswali kwa mashabiki na watu wanaomfuatilia.