Ijumaa , 26th Apr , 2019

Mwigizaji maarufu wa Bongo Movies, Riyama Ally amefunguka kuwa hapendi watu wanavyomuita mtu mzima, akisema yeye ni mdogo hasa kwa mume wake.

Riyama na mumewe

Akizungumza na eNewz ya EATV, Riyama amesema kuwa umri wake, muonekano wake na unene wake hauwezi kumzuia kufanya manjonjo kwa mumewe.

"Mimi kwetu mwili ni asili yetu, kwahiyo hata kama nikisema niache dawa na nikiacha tu hizo dawa nitarudi kwenye ubonge na hali niliyo nayo haiwezi kunizuia kuenjoy na mume wangu", amesema Riyama.

"Mapenzi sio wembamba wala unene, kuwa mtu mnene sio kushindwa na ndoa, sisi watu wanene ni kama oven, muda wote tunachemka", ameongeza.

Tazama hapa chini akizungumzia zaidi.