Alhamisi , 5th Mar , 2020

Msanii Aslay ameeleza kusikitishwa na vitendo vinavyopangwa na watu ili kumpakazia kama amempiga mzazi mwenziye aitwaye Sonia, baada ya kusambaa kwa taarifa ikieleza msanii huyo anatuhumiwa kufanya tukio hilo.

Msanii Aslay

Kwa kuthibitisha hilo Aslay amepost kipande cha sauti katika mtandao wa Instagram, akiwa anamuuliza mzazi mwenziye kama ni kweli amempiga kisha akaandika.

"Nimesikitishwa sana na vitendo vya kupangwa vyenye nia mbaya dhidi yangu, jioni ya leo wamesambaza video ikidai nimempiga mzazi mwenzangu ni habari ya kizushi mno, sijamgusa kwa namna yoyote ile, ninachokifahamu kuna watu walifika nyumbani kwangu na kuanza kufanya fujo kwa sababu zao" ameandika Aslay.

"Sitaongea mengi najua ukweli  utajulikana tu, kinachosikitisha sana kwangu na kwetu kama jamii, ni jinsi vyombo vya habari vinavyoweza kutumika kusambaza uongo, chuki na kuharibu majina ya watu na biashara zao ila Mungu pekee ndiyo shahidi wa ukweli" ameongeza. 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

Nimesikitishwa sana na vitendo vya kupangwa, vyenye nia mbaya dhidi yangu vinavyoendelea. Inasikitisha zaidi, Media (Online Media) inapojiingiza kwenye michezo michafu ya hovyo kwa faida nisizojua (yaweza kuwa wamepewa pesa au wana sababu zao nyingine). #GlobalOnline wamenikosea sana, sijui mtu anayeheshimika kama #EricShigongo anawezaje kuajiri watu wasio na weledi, wakaenda kushiriki kwenye habari za uzushi namna hii tena za kupangwa. Jioni ya leo wamesambaza video ya kupikwa, ikidai kwamba eti mimi nimempiga Mzazi mwenzangu (Sonia). Ni habari ya kizushi mno, sijamgusa kwa namna yoyote. Ninachokifahamu kuna watu walifika nyumbani kwangu na kuanza kufanya fujo kwa sababu zao, pengine ilikuwa kunilazimisha kufanya vitendo vya ajabu kwa hasira wakimtumia Sonia, na kumshawishi aseme uongo. Nashukuru Mungu sikufanya kitu chochote kibaya. . Nilimpigia Sonia kuuliza nini kimetokea, mwenyewe anashangaa japo anakiri wapo watu wanaomshawishi kuongea uongo mwingi kuchafua jina langu. . Sitaongea mengi, najua ukweli utajulikana tu. Kinachosikitisha sana kwangu na kwetu kama jamii, ni jinsi vyombo vya habari vinavyoweza kutumika kusambaza uongo, chuki na kuharibu majina ya watu na biashara zao. Walioko nyuma ya michezo hii michafu tunawafahamu, na wao wananifahamu, wakati utawambua, NA MUNGU PEKEE NDIYE SHAHIDI WA KWELI. . Asanteni

A post shared by Aslay (@aslayisihaka) on