Jumanne , 9th Jul , 2019

Michael Adams, Mkazi wa nchini Marekani anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kesi ya mauaji ya kijana mwenye umri wa miaka 17, kwa kumpiga na kumkaba hadi kufariki kwa sababu ya kusikiliza muziki.

Kushoto ni marehemu na kulia ni mtuhumiwa wa kesi ya mauji

Polisi wamesema tukio hilo limetokea katika eneo la Circle K , Peoria ave lililopo nchini Marekani, na mtuhumiwa mwenyewe Michael Adams amekiri kufanya tukio hilo na amewaambia maofisa wa polisi sababu ni marehemu alikua anacheza na kusikiliza muziki wa rap.

Kijana huyo alikua anasikiliza muziki wa rap, na aina ya muziki huo unamfanya yeye kutokuwa salama na ameshambulia watu wengi ambao wanasikiliza muziki huo”, amesema mtuhumiwa huyo.

Aidha mwanasheria wa mtuhumiwa huyo amesema amemtetea mteja wake kuwa alikua anasumbuliwa na ugonjwa wa kiakili na aliachiwa kutoka jela siku 10 zilizopita kabla kufanya tukio hilo.

Walimuachia kurudi mtaani bila ya kumpima afya yake, tiba na hata kumuwekea ulinzi. Huko ni kushindwa kwa idara hiyo na inatakiwa kufanyiwa marekebisho”.