Jumatano , 4th Mar , 2020

Nabii wa kike huko nchini Nigeria ambaye ametambulika kwa jina la Patience Akpabio, amewashauri wanawake kutolala na wanaume zao gizani kwa sababu wanazalisha watoto ambao wanakuwa na mtazamo tofauti duniani.

Nabii Patience Akpabio

Nabii huyo amezua gumzo mitandaoni nchini Nigeria, baada ya kutoa angalizo hilo katika mtandao wa Facebook, ambapo amewakataza wanawake kutofanya mapenzi gizani kwa sababu watoto wanaozalishwa wanakuwa hawana mitazamo chanya na yenye nguvu.

"Huu ni mwaka 2020 hakuna kufanya mapenzi gizani, ukiwa na mume wako taa zinatakiwa ziwe wazi, watoto wanaozalishwa wakati mnafanya tendo huku mkiwa gizani, wanakuwa na maono tofauti ya kidunia kuliko wale waliozaliwa kipindi kuna mwanga wa taa" ameandika Nabii Patience Akpabio.