Akizungumza na www.eatv.tv, Tunda amesema pete hiyo akutarajia kwa kuwa ilikuwa ni 'suprise', hivyo watu wakae mkao wa kula kushuhudia harusi yake na mpenzi wake huyo ambaye hajataka kumtaja.
“Ni pete ya uchumba, ilikuwa suprise mwenyewe nilikuwa sifahamu, mahari bado na wala sijui itakuwa ni bei gani, ndo naolewa kweli wasubiri tu waone ndoa ndani ya mwaka huu inshallah”, amesema Tunda.
Msichana huyo ambaye aliwahi kuwa kwenye mahusiano na rapper Young D, amesema kwamba kwa sasa ameamua kubadilika na kutulia, ili aweze kumudu ndoa yake.