Twitter wamesema kwa sasa wanaondoa uwezo wa mtu kuweza 'ku-tweet' kupitia njia ya ujumbe mfupi ambayo ili ifanye kazi lazima uunganishe namba yako ya simu na akaunti yako ya Twitter.
Inaelezwa kuwa, njia iliyotumiwa na wadukuzi kudukua akaunti ya Jack Dorsey ni namba yake ya simu na wadukuzi hao walianza kutuma ujumbe kadhaa katika akaunti yake bila kuingia katika akaunti kwa njia zilizozoeleka kama tovuti au 'application' maalum ya Twitter.
Twitter walipojulisha umma kuhusu mabadiliko hayo.
Mpango huo una dhumuni la kuifanyia marekebisho zaidi ili kuleta usalama ila hawajasema lini watairudisha tena lakini wachunguzi wa masuala ya teknolojia wanaona huenda wakaleta uwezo wa kuhakiki mara mbili zaidi (Two factor authetication), kupitia uwezo huo wa namba japo bado haiwezi kuwa ndiyo tiba ya usalama moja kwa moja.