Jumapili , 2nd Apr , 2017

Ikiwa joto limepamba moto katika Ligi Kuu Tanzania Bara leo hii timu ya Afrika Lyon imeweza kujinyakulia 'point' 3 baada ya kuichapa Stand United  bao 1-0 katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam na kuifanya klabu hiyo kuwa kupanda nafasi nne kuu 

African Lyon vs Stand United

Goli hilo limefungwa na mshambuliaji wake pembeni Abdallah Mguhi ‘Messi' katika dakika 23 ya kipindi cha kwanza ya mchezo na kuweza kuiandikia timu yake bao la pekee

Kufuatia ushindi huo, Afrika Lyon imeweza kupanda juu katika msimamo wa Ligi kuu mpaka kufikia nafasi ya 9 ikiwa na point 29 ambapo awali ilikuwa katika nafasi ya 13 kwa pointi 26.

Ikumbukwe kuwa Abdallah Mguhi 'Messi' ndiye aliyechungulia nyavu za timu ya Simba SC katika mzunguko wa kwanza na kutibua rekodi ya kutofungwa kwa Simba katika mzunguko huo.