Mbunge wa Mikumi Mh. Prof Jay
"Ngoja tuone kwanza ianze halafu baadaye ndiyo tutajua tuta-comment kitu gani kitakachoendelea lakini kwa mimi sioni kama itaenda kufanikiwa kwa sababu bahati nzuri au mbaya mkuu wetu wa mkoa amekuwa anaongea vitu vingi sana ambavyo havitekelezeki sasa nataka nione kwa hili amaejipangaje".
Prof Jay ameendelea kusema tunaweza kubeza kama haiwezekani baadae akafanikiwa ngoja baada ya muda tuone ana mipango gani na sasa hivi dunia imebadilika unahitaji kupata neno la Mungu mahali popote ila kwenye klabu itakuwa shuguli nzito sidhani kama linawezekana. amesema Prof Jay.
Aidha Prof Jay ameachia kazi yake aliyoshirikiana na ndugu zake wawili Black Rhyno, Donkoli, Mr Teacher na Simple X iitwayo kaza.