Andreas Pirlo akiwajibika katika kikosi cha vijana cha Juventus chini ya miaka 23
Pirlo ambaye ameteuliwa majuzi kuchukua nafasi ya kocha Maurizio Sarr aliyefutwa kazi baada ya kutolewa katika mashindano ya mabingwa na olympic lyon katika hatua ya 16 bora
Katika kusudio lake la kuijenga timu hiyo ataanzia marekebisho kwenye idara ya kiungo huku akitaka kumruhusu Aaron Ramsey kuondoka na kumtafuta kiungo mwingine bora zaidi ambapo Tony Kroos na Isco awanatajwa moja wapo kuhamia Juvetus toka Real Madrid
Kumekuwa na mjadala mkubwa juu ya uwezo wa Pirlo kakabidhiwa mikoba mikubwa ya Ukocha akiwa hana uzoefu wa kutosha katika nafasi hiyo licha ya kuwa mchezaji mahiri wakati wake