Chile ambayo kwa mashindano ya mwaka huu hawatakua na kocha Jorge Sampaoli wameorodheshwa katika kundi D na timu za taifa za Bolivia,Argentina na Panama.
Mabingwa mara nyingi wa michuano hiyo Uruguay wapo Kundi C na timu za Venezuela, Jamaica na Mexico huku Brazil ikiangukia kundi B lenye timu za Peru, Haiti na Ecuador nalo kundi A likiundwa na timu za U.S.A, Paraguay, Costa Rica na Colombia.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 03 mwaka huu ambapo Colombia itaumana na USA huko Santa Clara Calfornia.