Paul George katika majukumu yake dimbani
Terance Mann aliifungia Clippers ambao walikuwa nyuma kwa alama 25 katika robo ya tatu ya mchezo huo huku Paul George akifunga alama 28 na kucheza mipira ya kurudi mara 9 na assisti 7 akichagiza ushindi huo.
Ikumbukwe Clipers wameshinda mchezo huo bila ya uwepo wa nyota wao Kawhi Leonard ambaye kwa sasa ni majeruhi.
Katika fainali Los Angeles Clippers itakipiga dhidi ya Phoenix Suns.
Katika kanda ya Mashariki, Phidalelphia 76ers wamelazimisha sare ya 3-3 na Atalanta Hawks baada ya ushindi wa leo hivyo watacheza mchezo wa saba ili kupata mshindi.